HabariKimataifaNews

WHO yasema watu wasiopungua 137,000 huaga dunia kila mwaka kwa kuumwa na nyoka…

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kuwa, watu 81,000 hadi 137,000 hupoteza maisha kila mwaka katika maeneo mbalimbali duniani kutokana na athari zinazosababishwa na kuumwa na nyoka wenye sumu.

Tangazo hilo limetolewa katika hafla ya uzinduzi wa  jukwaa maalum mtandaoni kwa lengo la kutoa taarifa na kuelimisha umma kuhusu hatari ya kuumwa na nyoka wenye sumu na wapi waliko nyoka hao hatari zaidi duniani.

Aidha taarifa hiyo imeelezwa kwamba, mbali ya vifo vya watu hadi 137,000 kila mwaka, kuumwa na nyoka pia kumewaacha mamilioni ya watu na vilema vya maisha.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema, kuumwa na nyoka mwenye sumu kali kunaweza kusababisha kupooza ambako kunaweza kumzuia mtu kupumua, kumsababishia maradhi ya kutokwa na damu, matatizo ya figo yasiyoweza kutibika na kuharibu mishipa ambayo inapelekea ulemavu wa maisha na kukatwa viungo.

BY NEWS DESK