HabariLifestyleMakala

FAIDA ZA KUFUNGA SEHEMU YA PILI [KIROHO]

Kwa wale ambao wana utaratibu wa kufanya maombi kufunga kunawawezesha kutulia kwenye maombi na kuweka mawazo yao kwenye kile hasa wanachotaka kukamilisha kwenye maombi yao. Kama tulivyoona kwamba kushiba kunapoteza nguvu ya mwili, kufunga kunakufanya uwe na nguvu ya kuweza kufanya maombi muhimu kwako.

Pia wale ambao wanafanya tahajudi (meditation) kufunga kunawawezesha kudhibiti mawazo yao wakati wana tahajudi. Kwa sababu mwili hauna mzigo mwingine unaofanyia kazi ni rahisi kudhibiti mawazo yako na kuweza kufikiri kwa kina kile ambacho unataka kufikiri.
Kufunga pia kunakufanya uwe na shukrani, kitu ambacho ni muhimu kwenye ukuaji wa kiroho. Unapoweza kushukuru kwa kidogo unachopata unajiweka kwenye nafasi ya kupata kikubwa zaidi.