MichezoMombasaSports

Timu 32 Kutoka Kaunti Za Mombasa Na Kwale Kuwania Ubingwa Wa Makala Ya 6 Ya Rashid Abdalla Supercup.

Makala ya sita ya dimba la Rashid Abdhalla Supercup  hatimaye yamewadia huku  timu 32 zikitatarajiwa kuwania ubingwa wa mashindano hayo ya kipekee mwaka huu.

Mashindano hayo yatachukua muundo  mpya utakaojumuisha timu 32 ,16 kutoka Kaunti ya Mombsa na 16 kutoka Kaunti ya Kwale amabzo zimepangwa kwenye makundi manne mtawalia,  kila kundi likiwa na timu nne.

Hii ni kufuatia droo  iliyoandaliwa Jumatatau Mei 12 katika shule ya akademia ya Aghakhan mjini Mombasa ambayo iliweka bayana makundi yote.

Akizungmza baada ya kukamiika  kwa droo hiyo mwandalizi wa mashindano hayo Rashid Abdhalla alisisitiza azma ya kukuza vipaji katika ukanda wa pwani.

Abdalla amesema hatua ya kujumuisha timu kutoka kaunti hizo mbili n njia ya kutoa fursa sawia kwa timu kushiriki dimba hilo na kuhimiza umoja na ushindani kupitia soka.

Nina imani kwamba mwaka huu tutaona vijana wengi  wakipata fursa za kucheza mpira na kukuza vipaji vyao.

Kutakuwa na mawakala ambao watakuwepo kuwatizama vijana wetu kutoka haopa nchini na wengine  kutoka mataiofa ya nje ili wachezaji wapate nafasi pia ya kucheza sit u katika timu kubwa za hapa nchini bali pia vilabu kutoka nje.” alisem Abdalla

Rashid hata hivyo ametoa wito kwa timu zote zitakazoshiriki kudumisha nidhamu kwenye mashindano hayo ili kuwavutia wawekezaji zaidi.

“Nidhamu ndio kitu cha msingi na ikiwepo ndio amabapo wawekezaji watapata urahisi wa kuwekeza fedha zao.’” Abdallah alionya.

Kwa upande wake kocha wa zamani wa harambee stars Ghost Mulei amepongeza juhudi za kukuza vipaji kupitia mashindano hayo akisema yametengeneza njia kwa wachezaji wachanga kuonyesha vipaji.

Mulei ametambua eneo la pwani kama kitovu cha vipaji hasa katika ulingo wa soka na kuahidi kufanya kazi kwa ukaribu na wandalizi wa mashindano hayo kuhakikisha vipaji vinatambulika katika soka ya chini na hata kimataifa.

Tutafanya kazi na Rashid Abdalla wakati wa toleo hili ili kusaidia kutambua na kukuza vipaji bora. Coast ina baadhi ya wachezaji bora nchini, na wanastahili jukwaa la kung’ara,” alisema Mulei.

Makala ya sita ya kitufe hicho yanayatrarajiwa kuwa na ushindani mkubwa na mihemko ya aina yake na kutoa juwaa la kipekee kwa vijana kuendelea kukuza vipaji vyao.

MAKUNDI

Kwale

Kundi A

Denmark

Kundutsi

Green boys Mshale fc

Kundi B

Dumna

Generation United

Kinango Raptors

Nasty milan

Kundi C

Lazium

Fafada

Similani

Makamini combine

Kundi D

Azam Utd

Vivah Manyotta

Blue Rangers

Vanga Utd

Mombasa

Kundi A

Congo Boys

Shanzu Utd

Kishada Soccer

Wananyuki Fc

Kundi B

BandariYouth

Shimanzi Fc

Fayaz Bakers

Vimbwanga

Kundi C

Mombasa All Stars

Tononoka combine

Ziwani fc

Change Youth Academy

Kundi D

Paranja biro

Mvita young stars

Kiembeni rebels

Sparki youth

By Mohammed Mwajuba.