HabariNews

Justina Syokau ajibu madai kwamba gari alilozawadiwa si jipya.

Mwimbaji wa nyimbo za Injili Justina Syokau amejitetea baada ya kuwekwa wazi kuhusiana na gari alilozawadiwa siku yake ya kuzaliwa.
Mwimbaji huyo mwenye utata, kwenye ukurasa wake wa Instagram, alichapisha video ya wakati alipopokea gari aina ya Land Cruiser nyeupe na kuongeza maelezo yaliyotaja hali ya gari hilo kuwa 'mpya'.

“Mwaka umeanza na kupanuliwa mipaka. Ndani ya gari langu jipya la thamani ya mamilioni. Ni msimu wangu,” Justina aliandika.


Picha zilizoshirikiwa mtandaoni, hata hivyo, zilivuta hisia za watumiaji wa mtandao wenye macho makali ambao waliharakisha kusema kwamba usukani ulikuwa umechakaa.

Huku kukiwa na mtindo wa kuwinda mvuto miongoni mwa watu mashuhuri wa Kenya, baadhi ya mashabiki wake pia walimshutumu Justina kwa kutaka kuzingatiwa na Wakenya mtandaoni.

Wengine walipingana na ukweli kwamba mwimbaji hakutaja ni nani aliyempa zawadi hiyo.

"Wanandoa wanaoishi nje ya nchi walinipa zawadi ya gari. Sikutarajia. Wamekuwa wakisaidia miradi yangu na ni wafuasi wangu wakubwa," alisema.
Mama huyo wa mtoto mmoja pia alifichua kuwa gari hilo liligharimu zaidi ya KSh 20 milioni na alikuwa akitafuta dereva mzoefu.
 
"Ingawa ninaweza kuendesha gari hili, ninahitaji dereva aliye na uzoefu ambaye atakuwa mwangalifu na asiliangushe," alisema. 

Aliongeza kusema, "Ninahitaji kuajiri polisi wa kulinda lango langu kwa sababu gari hili ni ghali na siwezi kustahmili ikiwa litapotea." 

Akizungumzia kuhusu mwanamume wa miraba minne ambaye alionekana naye katika siku yake ya kuzaliwa, mwanamuziki huyo alisema, "Siko katika mahusiano na kijana huyo. Alitumwa kukabidhi gari na wanandoa walionitunuku zawadi."

BY EDWIN KIPROTICH