HabariLifestyleNewsSiasa

Serikali Kujenga laini ya umeme ya sh. Bilioni 66 kukabiliana na kukatika kwa nguvu za umeme

Rais William Ruto ameiagiza Wizara ya Nishati kushughulikia kwa kina changamoto ya kukatika kwa umeme.

Rais ambaye aliongoza kikao cha Baraza la Mawaziri siku ya Jumatano alisema kukatika kwa umeme mara kwa mara kunaathiri sifa ya Kenya ya uwekezaji.

Baraza la Mawaziri lilijadili suala hilo kwa upana na kuazimia kwamba mfumo wa njia za kusambaza umeme unapaswa kuunganishwa ili hitilafu ya umeme katika sehemu moja isiathiri nchi nzima.

Ili kukabiliana na upakiaji kupita kiasi wa laini za upitishaji umeme unaosababisha kukatika, laini ya Bomet-Narok itajengwa kwa Euro milioni 400 (KSh bilioni 66) kutoka kwa Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Laini hiyo iliyofadhiliwa mwaka 2016 haijajengwa kutokana na migogoro ya kisheria.

Zaidi ya hayo, mradi wa nishati ya jua wa Euro 1.2 (KSh200 bilioni) wa KenGen katika Bwawa la Seven Forks utatoa ulinzi dhidi ya kukatika kwa umeme.

Mradi huo wa Megawati 42 una hifadhi kubwa ya betri na nguvu inapokatika, nishati iliyohifadhiwa hutumika.

Fauka ya hayo, mradi huo unasaidia kuokoa nishati ya maji katika mabwawa matano yanayounda Seven Forks.

BY EDITORIAL