HabariNews

SERIKALI KUFANIKISHA MRADI WA NYUMBA ZA BEI NAFUU MOMBASA.

Serikali imesema imeweka makakati kabambe kufanikisha mchakato wa ujenzi wa nyumba

za bei nafuu kaunti ya Mombasa na Pwani kwa ujumla.

Akizungumza na wanahabari hapa Mombasa baada ya kikao na wadau husika, naibu kamishna wa

kaunti ya Mombasa Ronald Muiwawi alipigia upatu mradi wa ujenzi wa nyumba nafuu nchini akisema

utawasaidia wengi kupata makaazi yaliyobora kwa bei nafuu pamoja na kubuni nafasi za ajira.

 

Aidha alidokeza kuwa serikali imetambua sehemu kadhaa za kutekeleza miradi hiyo katika eneo la

pwani huku wakilenga kupata nyumba 50,000 eneo hilo pindi itakapokamilika.

“Tunalenga kujenga nyumba 50,000 kaunti hii ya Mombasa na tunatarajia kila kitu kitaenda kwa utaratibu

na kwamaba haya yote ambayo yameratibiwa yatakamilika na tunaomba wananchi na viongozi wa Mombasa

washirikiane na kamati husika na serikali kuu kuhakikisha mambo haya yanafanikishwa.Alisema Muiwawi.

 

Kwa upande wake John Karanja mkurugenzi wa mradi huo ukanda wa pwani ameweka wazi kuwa serikali

imekamilisha mchakato wa kuwafidia waliokuwa wakiishi eneo la Buxton.

Karanja alitoa hakikisho kuwa serikali imeweka mipango ya kuhakikisha wakaazi na wafanyabiashara wa kaunti

ambazo miradi hii inaendelezwa wamenufaika kikamilifu na suala hilo huku akihimiza wananchi kushirikiana na

viongozi kufanikisha hayo. “ili kuhakikisha kila mtu anafaidika na mradi huu umeorodhesha zaidi ya vifa 80,00

vitakavyohitajika na kuhakikisha kila mmoja anafaidi tumekuja na mradi wa kuandikisha wanajauakali, mafundi

na wengine wote watakaohusika na usambazaji wa vifaa hivi.” Alisema Karanja

 

Naye Suleiman Mwatsanga mkuu wa muungano wa wanajuakali eneo bunge la Likoni kaunti ya Mombasa

alipongeza mradi huo akisema utaimarisha maisha ya wengi kwa kuwawezesha kupata ajira na kukimu mahitaji yao.

“Kuja kwa ujenzi wa hizi nyumba kwa sababu watu wa jua kali wamewekwa kando wamedharauliwa hawatambuliki

kwa sababu hawana makaratasi,kazi zao hazina thamani lakini kwa sasa tunashuruku rais William Ruto kuleta hili

jambo na sekta ya hii itawafanya vijana wengi kujishughulisha na kukuza familia zao.” Alisema Mwatsanga.

By MEDZA MDOE